UPRISING


 



Vurugu Za Zanzibar; Taarifa Za Hivi Karibuni...


Jeshi la Polisi Zanzibar limelazimika kutumia Mabomu ya Machozi ili kuwatawanya wafuasi wa kikundi cha Uamsho waliokuwa wamekusanyika kufanya Dua ya kuwaombea watu waliokufa katika ajali ya kuzama kwa Meli ya Mv. Skagit katika Mitaa ya Mbuyuni.

Habari kutoka Zanzibar zinadai kuwa Jeshi hilo la Polisi lililazimika kutumia Mabomu ya Machozi kutokana na kikundi hicho cha Uamsho kuanza kuhubiri siasa badala ya kufanya Dua hatua iliyosabaisha kuvunjika kwa amani katika mitaa hiyo.

Mwandishi wa Kituo hiki cha Uhuru FM aliyeko Mjini Zanzibar amesema licha ya Watanzania kuendelea kuomboleza vifo vya watu waliokufa katika ajali hiyo, bado kikundi hicho cha Uamusho kimeendelea kufanya sisasa badala ya kufanya Dua.

Pia imeelezwa kuwa chanzo cha Mabomu hayo ya Machozi ni kikundi hicho kufanya Dua yenye utata huku masuala ya siasa yakijitokeza hatua iliyopelekea kuwepo kwa vurugu za hapa na pale hivyo Jeshi likaamua kutumia nguvu ya ziada ili kuwatawanya. 

CHANZO:  Radio  Uhuru FM
Reactions::

KWANZA JAMII IRINGA JUMA HILI!

Liko mitaani, Kihesa, Ipogolo, Mtwivila, Mwanyingo, Isimani na kwingineko.
Reactions::

JK Akiteta Na Rais Wa Zanzibar Na Makamu Wake

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Sheik na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal wakiongea katika Ikulu ya Zanzibar leo. Picha: IKULU

Reactions::

JK Aswali Swala Ya Ijumaa Na Dr Bilal

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal wakijumuika na wananchi wa Zanzibar katika swala ya Ijumaa katika msikiti wa Mwembe Shauri, Unguja. Picha: IKULU
Reactions::

Yanga Yaibamiza APR Mabao 2-0 Kombe La Kagame

Mchezaji wa timu ya APR ya Rwanda, Selemani Ndikumana akijiandaa kupiga mpira mbele ya beki wa timu ya Yanga, Kevin Yondan wakati wa mchezo wa kuwania kombe la Kagame uliofanyika leo kwenye uwanja wa Taifa katika mchezo huo Yanga wameitwanga APR mabao 2-0 yaliyofungwa na Said Bahanuz.


Kikosi cha timu ya APR kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa.


Kikosi cha timu ya Yanga kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa.
Chanzo: www.fullshangweblog.com
Reactions::

Taarifa Za Hivi Karibuni; Zanzibar Kumechafuka Tena!



Kuna vurugu zinaendelea Zanzibar. Tutwawaleteeni taarifa zaidi kadri tukavyozipokea.
Reactions::

Yakiporomoka Ni Stori Nyingine...!

Reactions::

WATEJA WA VODACOM WANUFAIKA NA OFA YA MWISHO WA WIKI

  • Manufaa ni kuhusu kupiga simu,kutuma ujumbe mfupi, na huduma ya hifadhi habari kwa Shs, 250/- tu
  • Manufaa ni kwa mwisho wa wiki kuanzia Ijumaa saa 5 usiku hadi Jumatatu saa 1 asubuhi.
Wateja wa Vodacom Tanzania wana sababu ya kufurahi kipindi cha mwisho wa wiki kufuatia kuanzishwa kwa huduma mpya ambayo itawaruhusu kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi kwa gharama ya Shs. 250/- tu.
Huduma hii ni kwa mwisho wa wiki kuanzia Ijumaa saa 5 usiku hadi Jumatatu saa 1 asubuhi kwenda mitandao yote.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Bw. Rene Meza huduma hii imekuja kufuatia kubaini kwamba watumiaji wa mtandao huu huhitaji huduma hizi kwa masaa mengi zaidi na wakati mwingine mpaka usiku mwingi.
“Tumekuja na huduma hii ili tuweze kuhakikisha kuwa tunawaridhisha wateja wetu na papo hapo wafurahi na wale wawapendao,” alisema Meza.
Mkurugenzi mtendaji huyo aliongeza kuwa Mtandao wa Vodacom Tanzania unaona faraja kwa wateja na hivyo kuwa na hali ya kuwapa upendeleo mahsusi wateja wake ili kuongeza idadi ya watumiaji.
Huduma hii inakuja wiki moja baada ya kampuni hii kuzindua huduma nyingine inayowalenga vijana wa Kitanzania ambayo inatilia mkazo wa matumizi ya mitandao ya kijamii.
“Wateja wetu tayari wananufaika na matumizi ya bure ya mtandao wa kijamii wa facebook, twitter na wikepedia kupitia huduma ya “phoneson kwa wajanja”. Pia tumeingia ubia na kampuni ya Nokia ili kuwawezesha vijana kupata huduma rahisi ya mtandao yaani Internet sambamba na mauzo ya bei ya chini ya simu aina ya ZTE ambazo zinauzwa hadi Shilingi 13,000/- yote hii ikiwa ni kutaka kuwapa raha wateja wetu,” alimalizia Bwana Meza

Reactions::

Nothing You Do For A Child Is Ever Wasted...!

Reactions::

Mama Mkwe Wangu Nimemsapraiz Na Hereni Ya ' Kilimanjaro Premium Lager!'!

 Na ameipenda kweli huku wengine wakimwonea wivu. Pongezi ziende kwa vijana wale wabunifu pale Dar waliobuni hereni hizi za vizibo vya bia ya Kilimanjaro, niwaambie, wakati nyumbani tunadharau vyetu, huku Ulaya hereni hizi zina soko la uhakika!
Reactions::

Nimetua Stockholm, Leo Futari Tunakula Wapi?



 Ndugu zangu,
Nimeingia Stockholm mchana huu. Nitakuwa hapa kwa siku tatu. Naama, Sthlm jua ni kali, na nanihii pia. Leo futari tunakula wapi? Nimekuja na  samaki wa maana kwa daku. Naam, miye napenda kuvua samaki.  Huko nilikotoka ukweni nimeshinda siku mbili nikivua samaki. Na mwanadamu unapovua samaki unatulia kimyaa, unatafakari pia.
Ramadhan Kareem!

Maggid Mjengwa,
0736 966032
Reactions::

Jenerali Ulimwengu: Nakisi Ya Usaili, Mtaji Wa Ushirikina

Hali hii ya kutokuthamini urithi wetu imetufanya sasa tutafute walezi wengine badala ya baba yetu, na walezi hawa ( ambao kwa hakika hawawezi kuwa na uchungu nasi) wanatuona kama “mazuzu” wa kutumiwa na watu wenye akili.

Wanatuona kama punguani kwa jinsi tunavyoweza kuendelea kuwa “omba-omba” miaka 50 baada ya Uhuru wakati tunazo rasilimali ambazo wao wanazimezea mate.
Nimewasikia, kwa mshangao mkubwa, watawala wetu wakitamka kwamba hawajui ni kwa nini nchi yetu ni masikini baada ya miaka yote hii na ikiwa na rasilimali zote hizi. Huko kutotambua ndiyo sababu mojawapo kubwa ya hali tuliyo nayo.

Haiyumkiniki kwamba mtu anaweza kugombea uongozi wa nchi au jamii, tena kwa juhudi kubwa na kwa kuahidi mambo lukuki, halafu baada ya kuwa ameingia madarakani akatangaza kwamba wakati wote huo alikuwa hajui matatizo ya jamii yake. Nini kilimsukuma kugombea?

Pasipo na shaka akilini mwangu, sababu moja kubwa iliyotufanya tukwame kiasi hiki imekuwa ni upuuzi wa uongozi na udhaifu wa watawala, vikiambatana na uwezo na utashi mdogo mno wa raia kuwasaili viongozi watawala wao na kusaili kila kilichowazunguka.

Tumefanikiwa kujenga jamii ya watu wasio na uwezo wa kusaili mambo ya msingi kabisa, na wasiotaka kuwasaili wale waliowakabidhi hatamu za uongozi, hata pale hao waliokabidhiwa hatamu hizo ni dhahiri kwamba wanazitumia vibaya; na matokeo yake ni kwamba wanawaumiza hao hao waliowaweka madarakani, na hao wanaoumizwa hawana la kufanya.

Kukosekana kwa utamaduni wa kusaili mambo yanayotuzunguka ndiko kunatufanya tuendelee kuamini kwamba binadamu anaweza kupaa kwa ungo; mwili wa albino una nguvu za miujiza; mtu anaweza kugeuka fisi na fisi akageuka mtu; kumbaka mtoto mchanga kunatibu Ukimwi…na ujinga mwingine wa aina hiyo.
Jamii isiyosaili mambo ni jamii ya wajinga, na wajinga wakisha kuwa wengi ndani ya jamii, hata weledi wachache ndani ya jamii hiyo hawafui dafu: watanyongwa.

Ndiyo maana tunapiga kelele siku zote kuhusu elimu bora, na elimu bora si ile ya kumeza “maarifa” bali ni ile inayomwezesha mtu kusaili mambo yanayomzunguka, kuuliza maswali ili apate majibu na kuuliza maswali kuhusu majibu anayopewa, na siku zote kuendelea kusaili hata yale mambo aliyodhani kwamba aliyaelewa awali. Ndivyo wenzetu walivyoendelea, na ndiyo sababu wako waliko nasi tunaendelea kurejea tulikotoka.
Bila shaka tunahitaji kuondokana na upuuzi na ujinga tulimozama iwapo tunataka kupiga hatua za kwenda mbele badala ya hizi za kurudi nyuma tunazozipiga kwa kasi leo hii (kwa sababu ni kweli tunarudi nyuma kwa kasi).

Mahali pa kuanzia ni mwanzo, na mwanzo daima  ni uongozi wa kisiasa. Siasa safi zitazaa mazingira safi ya watu kufanya kazi za kuleta maendeleo katika nyanja zote. Siasa hovyo zitajenga mazingira hovyo vivyo hivyo, ambayo yataendelea kutuzamisha katika upuuzi na ujuha.

Siasa zetu hazina budi kuwa na misingi ya usaili wa masuala yote yanayotuzunguka, na ziachane na unafiki wa wale wanaodhani kwamba kutosaili jambo au mtu ndio uaminifu na nidhamu.
Tukumbuke, wale wanaodhani viungo vya mwili wa albino vinaleta utajiri, au kwamba ungo ni helikopta, msingi wao mkuu ni kushindwa kusaili mambo na watu.

Katika siasa kushindwa kuwasaili wale waliokabidhiwa madaraka ya kuendesha jamii, au kushindwa kusaili miundo, mifumo na michakato inayoendesha jamii, ni ushirikina mwingine ambao matokeo yake ni kuidumaza jamii yetu. Htuna budi kupambana na dalili zo zote zinazotusukuma kutokomoea zaidi katika nakisi ya usaili.

Ndiyo maana napingana moja kwa moja na baadhi ya mambo yanayotamkwa na kufanywa na baadhi ya wakuu wa asasi za utawala nchini, ikiwa ni pamoja na wakuu wa shughuli za Bunge.
Ni kama vile wakuu hawa wa Bunge, pamoja na Spika na wasaidizi wake, wamo bungeni kuhakikisha watawala hawasailiwi, hawadadisiwi na hawakosolewi. Niliangalia kwa mshangao mkubwa ubishi kati ya 

Spika na mbunge aliyesema kwamba, pamoja na uzembe na upuuzi wa asasi nyingine, alibaini pia “udhaifu wa Rais,” na hili likawa ni tatizo kubwa lililositisha shughuli za Bunge kwa muda na likawa ni chanzo cha gumzo nchini.

Mimi najiuliza, iwapo mbunge wa upinzani atazuiwa kusema kwamba Rais, ambaye ni kiongozi wa chama tawala (ndiyo kusema chama anachokipinga mbunge huyo) ni dhaifu sasa aseme nini? Amsifu Rais kwa umahiri, ukakamavu na ushujaa? Apendekeze kwamba Rais abakie madarakani maisha, na chama chake kisipingwe? Kazi ya mbunge wa upinzani ni nini hasa?

Nadhani ni kutokana na ukali wa Spika kuhusu “udhaifu” wa Rais ndiyo ofisa mwandamizi serikalini akasimama bungeni kwa ukali kumshambulia mbunge aliyesema kwamba baadhi ya majaji hawafai na kwamba uteuzi wao ulikuwa wa kutiliwa shaka.

Ndipo nikatambua kwamba tunalo tatizo la msingi kuliko nilivyodhani mwanzo. Tatizo hilo ni la kifalsafa katika mfumo ambao msingi wake wa kidhana ni kwamba mkubwa hatiliwi shaka, na mambo yalivyo ndivyo yalivyo, na hakuna bora zaidi ya yalivyo.... Soma zaidi... http://www.raiamwema.co.tz
Reactions::

Maombolezo

Mjengwa Blog Imeguswa na msiba huu mkubwa kwa taifa letu sisi kama sehemu ya jamii nasi tunaomboleza siku 3 za maombolezo pamoja na watanzania wote kwa ujumla,hivyo tunaiweka blog yetu katika rangi yeusi  kwa siku 3 ikiwa ishara ya kuomboleza msiba huu wa ndugu zetu 
Kikosi kazi Mjengwa Blog
Reactions::

Vodacom Na Aina Mpya Ya Simu

Meneja Mkuu wa Nokia Tanzania Samson Mwajwala,akionesha aina ya simu ya Nokia Asha 200 inayouzwa kwa shilingi 149,999 pamoja na muda wa bure wa maongezi na MB 125.Simu ingine ya Nokia Asha 302 inauzwa kwa shilingi 219,000 wateja watapata MB 500 kwa miezi sita mfululizo baada ya kuweka muda wa maongezi wa Shilingi 1000, 2000, au 5000 huku huduma ya facebook, twitter na Wikipedia zikiendelea kuwa bure,katikati Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Vodacom Tanzania Bw. Mngopelinye Kiwanga na Meneja bidhaa wa Vodacom Elihuruma Ngowi.
Reactions::

Dagaa Kutoka Mwisho Reli...!

Reactions::

Biashara Ya Mbogamboga, Kasulu-Kigoma


Wajasiliamali wa mbogamboga (vitunguu na mazao mengine) Kijiji cha Bugaga, Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wakishindana kukimbilia wateja, waliokuwa wanapita na magari katika kijiji hicho. Chanzo: Daily Nkoromo Blog
Reactions::

Twisheni...!


Na: Elvan Limwagu wa www.limwagu.blogspot.com

Kutokana na tukio la vifo vya watu waliokunywa Pombe kali ya Gongo hivi karibuni, mimi binafsi napenda kuwaletea picha chache tu kuonyesha namna pombe hiyo inavyoandaliwa.

Kule kwetu Pombe hii huitwa kwa jina la NIPA wengine kwa kuipendezesha wakalirefusha jina hilo kuwa "New Internationa Pure Alcohol" na kwa hakika viongozi wengi waliotokana na makabila ya Wayao na Wamakuwa walisoma kutokana na ADA ya mapato ya pombe hiyo kali. 

Itakumbukwa kuwa kwa mara ya kwanza katika kampeni za uchaguzi za mwaka 1995 Mgombea moja alidiriki kuwaahidi wananchi wa makabila hayo kuwa wakimchagua ataruhusu pombe hiyo na kuiwezesha iwe inaandaliwa kitaalamu, ingawa kura hazikutosha.

Pombe ya Gongo au Nipa kule kwetu hutokana na Mabibo (tunda la mkorosho) ambalo hukaushwa juani na hatimaye kuweza kuhifadhiwa hata kwa zaidi ya miezi sita. Mabibo unayoyasikia yakishakauka hubadilika jina na kuitwa KOCHOKO ambazo inapofika wakati wake (ni baada ya msimu wa mauzo ya korosho kupita) hupatikana kwa adimu sana na waandaaji wake huitafuta hata kwa maili zaidi ya 60.

Kochoko hizo baada ya kuchambuliwa na kuondoa takataka hulowekwa kwa wiki nzima ndani ya pipa au mtungi (chungu kikubwa) na maji yake yakipata ladha ya juisi inayoweza kulevya (staili ya mnazi au ulanzi), ndipo huwa tayari kwa kupikwa kama unavyoona hizo picha.

Vifaa vilivyosababisha jungu hilo ni: Mtungi, mtutu uliounganishwa na ngalawa, chungu kidogo cha kufunika mtungi kwa ajili ya kuzua mvuke usitoke nje, udongo wa mfinyanzi kwa ajili ya kusiliba maunganisho ya mtungi na chungu na tundu la mtutu kutolea mvuke hadi kwenye chupa.

Mvuke unaotoka hupozwa ndani ya mtutu kwa maji baridi na kuwa maji yanayoitwa NIPA (Gongo). Ile Pure huitwa IPACHO ambayo ni Spiriti kabisa kwa kuwa inawaka wanapoijaribia wenyewe, ile ya mwisho inaitwa ALEKA ambayo kwa wanaojifunza huweza kuitumia. Ili kupunguza makali ya IPACHO huwa inachanganywa na ALEKA, hata hapo Konyagi ni cha mtoto.
Reactions::

Liganga...! (Jiwe)

Reactions::

Magazetini Leo Ijumaa









Reactions::

Safi Sana...!

Reactions::

Mnyika Kuwa Shahidi Kesi Ya Mauaji


MBUNGE wa jimbo la Ubungo, John Mnyika atakuwa ni mmoja wa mashahidi wa Serikali watakaoithibitishia mahakama namna walivyohusika washtakiwa wanaotuhumiwa kumuua Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Kata ya Ndago, Yohana Mpinga (30).

Jeshi la Polisi mkoani Singida, limemefikia azimio hilo baada ya kumhoji Mnyika kwa saa tatu juzi usiku, kuhusiana na tukio hilo la mauaji lililotokea baada ya mkutano wake wa hadhara uliofanyika Julai 14 mwaka huu, majira ya jioni.

Mahojiano hayo yaliyoanza saa 11.53 jioni na kumalizika saa 3:15 usiku, yaliendeshwa chini ya kikosi maalum cha askari wa upelelezi kutoka jijini Dar es Salaam kwenye ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilithibitisha kwamba Jeshi la Polisi lilimtaka Mnyika awe tayari kuitwa wakati wowote ili kusaidia kwenye kesi hiyo ya mauaji.

Tayari watu 18 wametiwa mbaroni, miongoni wakiwemo wanachama wa Chadema, kwa tuhuma za kuhusika kwenye mauaji ya kijana huyo wa CCM.


Mnyika alihojiwa huku akiwa na wakili wa Chadema na mbunge wa jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Mauaji hayo ya mwenyekiti wa UVCCM yalifanyika Julai 14 mwaka huu saa 10 jioni huko katika kijiji cha Nguvumali kata ya Ndago jimbo la Iramba magharibi.

Mauaji hayo yanadaiwa kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na vurugu zilizotokea kwenye mkutano wa hadhara ambao Mnyika alikuwa mgeni rasmi.

Katika hatua nyingine, mshauri na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitila Mkumbo, ambaye alikuwa ameambatana na Mnyika, alitarajiwa pia kuhojiwa kuhusiana na mauaji hayo jana.
Reactions::

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKA UJERUMANI

UMOJA WA WATANZANIA  UJERUMANI (UTU)

UNATOA MKONO WA POLE NA RAMBI RAMBI KWA NDUGU NA JAMAA WALIOPATWA NA MAAFA KUTOKANA NA AJALI YA MELI  MV SKAGIT ILIYOTOKEA ENEO LA CHUMBE  ZANZIBAR SIKU YA TAREHE 18.07.2012.

UMOJA WA WATANZANIA NCHINI UJERUMANI UMEPOKEA KWA MASIKITIKO MAKUBWA TAARIFA ZA AJALI MBAYA AMBAYO IMESABABISHA VIFO.

UMOJA WA WATANZANIA UNAUNGANA NA WATANZANIA WOTE NCHINI KATIKA KIPINDI HICHI CHA  MAOMBOLEZO.
MUNGU IBARIKI TANZANIA 
MUNGU UBALIKI UMOJA WA KITAIFA
  MFUNDO PETER MFUNDO
          MWENYEKITI WA
UMOJA WA WATANZANIA UJERUMANI (UTU)

Reactions::

MJENGWABLOG INATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO



KWA mara nyingine, Watanzania  tumepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kuzama kwa meli ya MV. Skagit iliyotokea jirani na kisiwa cha Chumbe, Unguja. Ndugu zetu wapatao 60 tayari wameripotiwa kupoteza uhai. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa letu.



Mjengwablog, kama chombo cha jamii cha habari na mawasiliano kinatoa salamu za rambirambi kwa  wahanga wote wa msiba huu mkubwa. Na  tunachukua fursa hii kumpa mkono wa pole  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa  Dr.  Jakaya Mrisho Kikwete, vivyo hivyo, mkono wetu wa pole umfikie Mheshimiwa Dr. Ali Mohammed Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Ya Zanzibar.

Mjengwablog inaungana na Watanzania wote katika siku hizi tatu za maombelezo kwa kutorusha habari na picha za matukio yenye kuashiria sherehe na burudani.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania.
Maggid Mjengwa
Mtendaji Mkuu, Mjengwablog.com
Reactions::

Ajali Ya Meli Zanzibar; Taarifa Za Hivi Karibuni....

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

WIZARA YA HABARI UTAMADUNI UTALII NA MICHEZO

Tel: 0255 24 2237325/0255 24 223 7313
Maelezo
Fax: 0255 24 2237314
E-mail:habarimaelezo@yahoo.co.uk, maelezozanzibar@zanlink.com
maelezozanzibar@hotmail.com, maelezozanzibar@gmail.com

TAARIFA YA SMZ KUHUSU AJALI YA MELI YA MV. SKAGIT ILIYOTOLEWA
USIKU HUU JULAI 19,2012

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetoa taarifa usiku huu ikieleza idadi ya watu waliopatikana
wakiwa hai ni 146 na kupata maiti 62.

Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari usiku leo,Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali
Ali Juma Shamuhuna alisema taarifa hiyo ndio sahihi na kuwataka wananchi kutoamini taarifa
zinazotolewa na watu wengine zaidi ya Serikali.

Waziri Shamuhuna alisema kwamba maiti 62 walipatikana ambao kati ya maiti hizo watoto ni
9 na kuna raia mmoja wa kike wa kigeni ambaye hakuweza kutambulika Uraia wake,lakini
umeonekana picha yake moja ndogo ya hati ya kusafiria.

Waziri Shamuhuna alisema meli hiyo ilibeba jumla ya abiria 290 kati ya hao watu wazima 250,
watoto wadogo 31 na mabaharia 9.

Waziri huyo aliwataka wananchi katika sehemu mbalimbali hasa katika vijiji vilivyo
kandokando ya bahari watakapoona maiti au mtu akiwa hai ambaye wanadhani ni wa ajali ya
Meli ya Skagit.

Aidha, Waziri Shamuhuna alisema kwamba kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam ambao
watakuwa na wasiwasi wa kutowaona ndugu na jamaa zao amewataka kufika Ofisi ya Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kupata taarifa zaidi au kuripoti habari za kupotelewa kwa
ndugu au jamaa zao.

Kwa upande wa Zanzibar, Waziri huyo aliwataka wananchi kufika kwa Masheha wao kutoa
taarifa kama hizo.

Serikali imewashukuru makampuni binafsi za usafiri baharini kwa msaada wao na wasisite kutoa
msaada katika kazi inayoendelea ya kutafuta watu au maiti wengine katika eneo la tukio.

Meli ya Mv. Skagit ilizama Julai 18,2012 karibu na Kisiwa cha Chumbe umbali wa maili sita
kuelekea Kusini mwa Kisiwa kidogo cha Yasin Zanzibar ikitokea Bandari ya Dar es Salaam
ilikoanza safari saa 5:30 asubuhi.

Meli hiyo inamilikiwa na Kampuni ya Sea Guall Sea Transport Ltd, Kampuni ambayo Meli yake
nyengine ya Mv. Fatih ilizama ikiwa Bandarini Malindi Zanzibar na kufariki watu sita mwaka
2009.

IMETOLEWA NA:
IDARA YA HABARI(MAELEZO) ZANZIBAR
ZANZIBAR, TANZANIA
JULAI 19,2012
Reactions::

Mjumbe; " Mwenyekiti, Umekuwa Kimya Sana Hadi.....!"



Mr.Chairman-Bado uko ukweni??Umekuwa kimya sana hadi blog inaanza kudorora. David V

Jibu:

Asante sana David,

Ni kweli, nimekuwa kimya. Huku nilipo mawasiliano pia ya tabu. Ni ya kuvizia tu. Lakini natumia muda huu kufanya niyapendao, ikiwemo hili la kuvua samaki. Unapovua samaki unatulia, unakaa kimya, unatafakari kwa kina pia.
Hata hivyo nitajitahidi kuwarushia yale niwezayo kuyarusha. 

Maggid,
Sweden
Reactions::

" Jamani Eee, Mwenyekiti Afyeka Majani Ukweni!"

Reactions::

Ni Zaidi Ya Kitonga...!

 

 

 

 

 

Tawi la Chadema Washington DC limepokea Mwanachama Mpya Ambae Pia Amezawadia Tawi Hilo Zawadi Ya Gari Ili Kufanikisha Shuhuli Za Chama Hicho






Mwenyeketi wa tawi la Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi, pamoja na katibu wake Mhe. Libe Mwang'ombe wakimkabidhi rasmi Hussein Kauzel Msabaha kadi ya uwanachama.


              Hussein Kauzel Msabaha akiwa na kadi ya Chadema


               Daftari la Sera ya Chama  Cha Demokrasia CHADEMA


Hussein Kauzel Msabaha akimkabidhi funguo za gari Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi


 Wanachama wa tawi la chadema Washington DC wakipata picha ya pamoja


Hussein Kauzel Msabaha akimkabidhi funguo za gari Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi.


Mwenyeketi wa Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC Mhe. Kalley Pandukizi akionyesha funguo za gari ya aina ya Chevy Suburban walilokabidhiwa na Hussein Kauzel Msabaha

 
Gari ya aina ya Chevy Suburban walilozawadiwa  Chadema na Hussein Kauzel Msabaha
Siku ya Jumamosi Juni 23, 2012, Tawi la Chama Cha Demokrasia CHADEMA Washington DC lapokea zawadi ya gari aina ya Chevy Suburban kutoka kwa Hussein Kauzel Msabaha, baada ya kukabidhiwa rasmi kadi ya uwanachama mpya wa chama hicho jijini Washington DC
kiongea katika hafla hiyo Mwenyekiti wa Chadema Washington DC Ndugu Kalley Pandukizi amemshukuru sana mwanachama wao huyo mpya na kusema gari hilo litawasidia katika kueneza Sera za Chama kwa Watanzania Wanaoishi Majimbo mengine ya Marekani.
Naye mwanachama huyo mpya amesema amejitolea gari lake hilo litumike kwa kazi za chama kwa Ridhaa yake si kwa kushawishiwa na mtu yeyote kutokana na kukubali Sera za Chadema. Mwenyekiti wa Chadema aliongeza kwa kusema anawaomba Watanzania wote wenye kutaka Mabadiliko waige mfano wa Ndugu Hussein Kauzela kwa kukisaidia Chama kwa hali na mali ili waweze kuzidi kukijenga Chama ambacho Wanachama wake ndio washika Dau wakuu kwenye kukijenga Chama.
Picha na Habari na Mdau SwahiliVilla

Chanzo: Haki Ngowi; http://www.blogger.com